Showing posts with label NEWS. Show all posts
Showing posts with label NEWS. Show all posts

Friday, April 28, 2017

US: Mfumo wa kujilinda ''utamuamsha'' rais wa K. Kaskazini

Upelekaji wa mfumo wa kujilinda dhidi ya makombora nchini Korea Kusini ulipingwa na waandamanajiHaki miliki ya pichaAFP
Image captionUpelekaji wa mfumo wa kujilinda dhidi ya makombora nchini Korea Kusini ulipingwa na waandamanaji
Mfumo wa kujilinda dhidi ya makombora wa Marekani unaowekwa nchini Korea Kusini utaanza kufanya kazi katika siku chache zijazo, jeshi la Marekani limesema.
Mfumo huo wa Thaad umetengezwa kuilinda Korea Kusini na majeshi ya Marekani yaliopiga kambi nchini humo dhidi ya vitisho vya Korea Kaskazini.
Vifaa vya mfumo huo vilipelekwa katika taifa hilo siku ya Jumatano, Admirali Harry Harris ambaye ni ni kamanda wa eneo la Pacific alisema kuwa Thaada itaanza kufanya kazi katika siku chache zijazo ili kuiinda Korea Kusini dhidi ya vitisho vya jirani yake Korea kaskazini.

Wanafunzi wanaopata ujauzito waendelee kusoma – Waziri Mwalimu

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia ,Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu amesisitiza kuwa wanafunzi wa kike wanaopata mimba wakiwa mashuleni waendelee na masomo yao, ili kufikia malengo walioyanayo nchini.
Waziri Ummy ameyasema hayo leo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kwanza wa masuala ya kijinsia ulioandiliwa na Chuo Cha Ualimu (DUCE) alipomuwakilisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano waa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.
“Tunapokataza watoto wa kike wasiendelee na masomo pindi wanapopata ujauzito wakiwa mashuleni, tunawaadhibu watoto wa masikini washindwe kutimiza malengo yao kwa wakati waliotarajia,”alisema Waziri Ummy.
Kwa upande wa Mkuu wa Chuo cha DUCE, Profesa William Anangisye amesema lengo la mkutano huo ni kuleta chachu ya kuwatia moyo wanafunzi wa kike kupenda masomo ya sayansi ili kupata wanasayansi wanawake nchini.

Marekani kuimarisha vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini

Taifa la Korea kaskazini limekuwa likitoa picha kuhusu zoezi la kijeshiHaki miliki ya pichaAFP
Image captionTaifa la Korea kaskazini limekuwa likitoa picha kuhusu zoezi la kijeshi
Mamlaka ya rais Donald Trump imewaelezea maseneta wote 100 wa bunge la taifa hilo kuhusu tishio la Korea Kaskazini na kubaini mikakati ya kuishinikiza Pyongyang kupitia vikwazo vya kiuchumi na vile vya kidiplomasia.
Lengo ni kuilazimu Korea Kaskazini kusitisha mpango wa makombora ya masafa marefu pampja na ule wa Kinyuklia.
Mwandishi wa BBC mjini Washington anasema kuwa mkakati muhimu pia utakuwa kuirai China kuishinikiza Pyongyang.
Maseneta wa Marekani walielezwa na mamlaka ya rais Trump kuhusu tishio linaloletwa na Korea KaskaziniHaki miliki ya pichaEPA
Image captionMaseneta wa Marekani walielezwa na mamlaka ya rais Trump kuhusu tishio linaloletwa na Korea Kaskazini
Seneta mmoja alisema kuwa habari hiyo kuhusu Korea Kaskazini ilikuwa muhimu sana.
Taarifa iliotolewa kwa niaba ya wizara ya Ulinzi na ile ya kigeni ilisema kuwa Marekani bado itaendelea na mazungumzo lakini imejiandaa kujitetea pamoja na washirika wake.

WAPINZANI NCHINI KENYA WAMPA ODINGA

Raila Odinga
Muungano wa vyama vya upinzani nchini Kenya National Super Alliance (NASA) umemteua aliyekuwa Waziri Mkuu Raila Odinga kuwa mgombea wake katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Agosti mwaka 2017.
Bw Odinga sasa atakabiliana na Rais Uhuru Kenyatta atakayetumia chama cha Jubilee kuwania muhula wa pili.
“Hii ni heshima kubwa sana ambayo ndugu zangu wamenifanyia, kwa kuniweka nipeperushe bendera ya NASA.Tumekuwa na vikao ambavyo vimechukua siku nyingi. Kila kitu tumeandika, tumekubaliana ya kwanza serikali tutakayoiunda, ambayo ni serikali ya mseto itakuwa ni serikali ya mpito,” alisema Bw Odinga akihutubu baada ya kutangazwa kuwa mgombea.
Amesema atakuwa kama Joshua kwenye Biblia na kuvusha Wakenya hadi nchi ya ahadi.
“Sisi tuko kama timu, yenye pembe tano (Pentagon), wamenipa utepe wa nahodha, hiyo inaniunganisha mimi nao na Wakenya wote, tutatembea pamoja bega kwa bega. Tunataka kubadilisha Kenya na kutekeleza ndoto ya waanzilishi wa taifa letu”.
Alisema serikali yake itaangazia kumaliza umasikini, kuimarisha afya, kuboresha uchumi, kubuni nafasi za kazi na kurejesha gharama ya elimu na maisha chini.
Bw Odinga pia ameahidi kuhakikisha walimu na madaktari,pamoja na wafanyakazi wengine wanalipwa mishahara mizuri.
Kadhalika, ameahidi akishinda serikali yake itamaliza rushwa serikalini.
Makamu wa rais wa zamani Musalia Mudavadi amesema viongozi wote wakuu wa muungano huo wamekubalina kumuunga mkono mgombea huyo mmoja.
“Tumekubali kwamba mpangilio huu wa uongozi ni mpangilio ambao tunataka ulinganishwe na Rasimu ya Bomas ambayo Wakenya walitaka, lakini haikuidhinishwa,” amesema.
Amesema mpango wao ni kuwa wadhifa wa kinara wa mawaziri na msaidizi wake, kama ilivyokuwa kwenye rasimu hiyo ya katiba.

Thursday, April 27, 2017

Atakaye vunja Muungano atavunjika yeye - Magufuli

 
Rais Dk. John Pombe Magufuli, leo amewaongoza Watanzania katika maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Rais Dk. John Pombe Magufuli, leo amewaongoza Watanzania katika maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulioasisiwa na Hayati Mwalimu Julias Kambarage Nyerere na Hayati Mzee Abeid Aman Karume mwaka 1964.
Wakati akihotubia Rais Dokt. John Magufuli amewasii watanzania kuendelea kudumisha na kuimarisha Muungano baina ya Tanzania na Zanzibar ulijengwa na waasisi wa taifa hili huku akisisitiza kuwa atakayethubutu kujaribu kuvunja Muungano huo atavunjika yeye.
Rais Magufuli ameyasema hayo pindi alipokuwa anahutubia wananchi katika kilele cha maadhimisho ya sherehe za Muungano zilizofanyika kwa mara ya kwanza katika uwanja wa Jamhuri, Jijini Dodoma kwa kusema kila mtanzania anaowajibu wa kulinda Muungano uliopo na kusisitiza kwamba njia pekee ya kuulinda ni kuchapa kazi kwa bidii.
"Mimi na mwenzangu Dkt. Shein tutafuta nyayo za wenzetu waliotutangulia kulinda Muungano huu kwa nguvu zote.... Asitoke mtu yoyote akajaribu kutaka kuuvunja Muungano wetu maana atavunjika yeye". Alisema Rais Magufuli
Pamoja na hayo, Rais Magufuli amesema kupitia Muungano kuna mafanikio mengi yamepatikana kutoka na juhudi za viongozi wa taifa na waasisi wa Muungano huo huku akipiga kijembe kwa kusema 'ukiona vyaelea ujue vimeundwa'

Jukwaa la Wahariri (TEF) lamshukia Profesa Lipumba


Profesa Ibrahim Lipumba
Jukwaa la Wahariri nchini (TEF) limelaani kitendo cha waandishi wa habari kujeruhiwa katika tukio la uvamizi lililotokea katika mkutano wa CUF katika hotel ya Vina kata ya Mabibo ambapo waandishi wa habari walipigwa na kujeruhiwa
Katika taarifa hiyo ya (TEF) imemtaka Profesa Lipumba kujitokeza na kukiri na kuomba radhi kwa waandishi wa habari pamoja na Watanzania kufuatia tukio hilo kama alivyofanya Maalim Seif 
"Tunamtaka Profesa Lipumba binafsi atoe kauli kuhusu tukio hili kama alivyofanya Maalim Seif ambaye binafsi aliandika barua rasmi kwa uongozi wa TEF akilaani kupigwa kwa waandishi wa habari na kutoa pole kwa wale waliomizwa na kupata mshtuko" Walisema viongozi wa TEF 
Taarifa hiyo ya TEF ilikwenda mbali zaidi na kuwatahadharisha waandishi wa habari, wahariri kuwa wanapaswa kuwa makini pindi wanapokuwa wanaitwa na kundi hili la Lipumba kwa ajili ya kutoa habari zao 

CCM bado ni chama bora - Nape Nnauye


Mbunge wa jimbo la Mtama, Mh Nape Nnauye akiwa na Rais Magufuli kipindi cha kampeni za uchaguzi Mkuu 2015.
Ikiwa leo Tanzania inatimiza miaka 53 toka Tanganyika na Zanzibar zilipoungana mwaka 1964 na kuunda nchi ya Tanzania Mbunge wa jimbo la Mtama, Mh Nape Nnauye amefunguka na kusema CCM ndiyo waasisi wa Muungano huo.
Mhe Nape Nnauye anakiri kuwa licha ya mapungufu ya hapa na pale katika chama chake hicho lakini bado kinabakia kuwa chama bora cha mfano barani Afrika, Nape Nnauye amesema hayo kupitia ukurasa wake wa Twitter 
"CCM bado ni Chama bora cha mfano kwa Afrika! Ni imara na kina historia ndefu, nzuri iliyotukuka sana! Ndio waasisi wa Muungano Wetu, tuudumishe" alisisitiza Nape Nnauye 

Rais Magufuli atoa msamaha kwa wafungwa


Rais Magufuli
Katika kuadhimisha Miaka 53 ya Muungano wa Tanzania ambayo sherehe zake za kitaifa zilifanyika Dodoma, Rais John Magufuli ametoa msamaha kwa wafungwa 2,219, imeelezwa. 
Tarifa ya Meja Jenerali Projest Rwegasira, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ilisema wafungwa hao ambao watafaidika na msamaha huo, wataachiliwa huru. 
"Ni mategemeo ya Serikali kwamba watarejea tena katika jamii kushirikiana na wenzao katika ujenzi wa Taifa na kwamba watajiepusha kutenda makosa ili wasirejee tena gerezani," taarifa ya Jenerali Rwegasira kwa vyombo vya habari ilisema.
Msamaha huo, hata hivyo hautahusu baadhi ya makosa na taarifa ya Katibu Mkuu iliorodhesha wafungwa wafuatao kutohusika nao:
Wafungwa waliohukumiwa adhabu ya kunyongwa na waliohukumiwa adhabu ya kunyongwa na adhabu hiyo kubadilishwa kuwa kifungo cha maisha au kifungo gerezani.
Aidha, msamaha hautawahusu wafungwa waliohukumiwa kifungo cha maisha gerezani, wanaotumikia kifungo kwa makosa ya kujihusisha na usafirishaji na matumizi ya madawa ya kulevya na wanaotumikia kifungo kwa makosa ya kujihusisha na uombaji na upokeaji au utoaji rushwa.
Wengine ni wafungwa wanaotumikia kifungo kwa makosa ya unyang’anyi na unyang’anyi wa kutumia silaha au kujaribu kutenda makosa hayo.
Msamaha wa Rais Magufuli pia utawapitia pembeni wafungwa wanaotumikia kifungo kwa makosa ya kupatikana na silaha, risasi au milipuko isivyo halali, taarifa hiyo ya Wizara ilisema.
"Wafungwa wanaotumikia kifungo kwa makosa ya shambulio la aibu, kunajisi, kubaka na kulawiti au kujaribu kutenda makosa hayo," ilisema taarifa ya 
Jenerali Rwegasira, hawatuhusika na msamaha wa Rais Magufuli.
Mbali na hao pia watu wengine ni 
"Wafungwa waliopatikana na hatia na kuhukumiwa kifungo kwa kosa la kuwapa mimba wanafunzi wa Shule za Msingi na Shule za Sekondari na ambao 
walitenda kosa hilo wakiwa na umri wa miaka 18 na kuendelea.
"Wafungwa wanaotumikia kifungo kwa makosa ya wizi wa magari na pikipiki, uharibifu wa miundombinu au kujaribu kutenda makosa hayo.
"Wafungwa wanaotumikia kifungo chini ya Sheria ya Bodi ya Parole (Act. No. 25/1994) na Sheria ya Huduma kwa Jamii (Act. No. 6/2002).
"Wafungwa waliopatikana na hatia na kuhukumiwa kifungo kwa makosa ya kutumia vibaya madaraka yao.
"Wafungwa waliowahi kupunguziwa kifungo na msamaha wa Mheshimiwa Rais na bado wangali wanaendelea kutumikia sehemu ya kifungo kilichobaki. 
"Wafungwa waliopatikana na hatia na kuhukumiwa kwa kosa la kuzuia watoto kupata masomo.
"Wafungwa waliopatikana na hatia na kuhukumiwa kwa kosa la utekaji wa watoto, kupoka na kufanya biashara ya binadamu.
"Wafungwa waliopatikana na hatia na kuhukumiwa kwa kosa la kukutwa na viungo vya binadamu.
"Wafungwa wanaotumikia vifungo kwa makosa ya kujihusisha kwa namna yoyote ile na nyara za Serikali na ujangili.
"Wafungwa wanaotumikia vifungo kwa makosa ya wizi/ubadhirifu wa fedha za Serikali.
"Wafungwa wanaotumikia vifungo kwa makosa ya kutoroka au kujaribu kutoroka chini ya ulinzi halali.
"Wafungwa walioingia gerezani baada ya tarehe 16/03/2017.
"Wafungwa warejeaji wa makosa/wafungwa waliowahi kufungwa gerezani."

Unga wamchanganya Zitto Kabwe


Mbunge Zitto Kabwe.
Mbunge wa Kigoma mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo Mhe. Zitto Kabwe amefunguka na kusema bei ya unga wa ugali sasa ni juu kuliko hata bei ya mafuta ya magari jambo ambalo linafanya wananchi kuumia na gharama hizi za chakula.
Zitto Kabwe amesema hayo kupitia mtandao wake wa Facebook na kusema bei hizi za chukula zipo juu sana na kufanya wananchi kuingia kwenye umasikini  
"Bei ya Unga wa Sembe 1kg TZS 2,300/= ( wastani ). Bei ya Mafuta ya Petroli 1lita TZS 2,060/= ( wastani). Kwa mara ya kwanza Ugali umekuwa ghali kuliko mafuta ya gari. Gharama hizi za maisha Kwa wananchi ni kubwa mno, hazistahmiliki na zinaingiza raia wengi kwenye umasikini. Serikali ipo kimya kana kwamba kila kitu kipo sawa" alisema Zitto Kabwe 

Wednesday, April 26, 2017

Mbunge Halima Mdee akubali yaishe


Mbunge wa jimbo la Kawe, Halima Mdee.
Mbunge wa jimbo la Kawe kwa tiketi ya CHADEMA Mhe. Halima Mdee jana amefunguka na kuomba radhi bungeni kufuatia kutoa lugha isiyokuwa na staha bungeni wakati wa uchaguzi wa Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki uliofanyika April 4, 2017.
Halima Mdee wakati akiomba radhi hiyo anasema kuwa siku hiyo ya uchaguzi kulikuwa na matukio ambayo yalikuwa yakiendelea bungeni ambayo yalimpelekea kutoa lugha isiyokuwa sawa kitamaduni za bunge, ambayo ilimgusa Spika wa Bunge na Naibu waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Khamis Kigwangala
"Mhe. Mwenyekiti tarehe 4 mwezi wa 4 wakati wa uchaguzi wa EALA kuna matukio ambayo yalikuwa yanaendelea yakanipelekea kuzungumza lugha ambayo kitamaduni za Bunge si sawa na lugha husika ilimgusa Spika wa bunge na Mhe, Kigwangala kwa namna moja au nyingine kama mbunge mzoefu nilitumia jitihada binafsi kuzungumza na kuomba radhi wahusika katika 'individual capacity'lakini vilevile nikaona ni busara kwa sababu haya maneno niliyasema bungeni hivyo kuzungumza pia hapa na kumuomba radhi Mhe. Spika kwa hiyo niliomba huu muda kwa lengo la kumuomba radhi, kumwambia namuheshimu na kumwambia sitarudia" alisema Halima Mdee 
Mbali na hilo Halima Mdee aliendelea kuomba radhi kwa wabunge, watanzania pamoja na wananchi wa jimbo la Kawe lakini pia Halima Mdee alisisitiza kuwa michango yake ya bunge itaendelea kama kawaida yake lakini kwa kutumia lugha za staa.    

Tuesday, April 25, 2017

Kero za muungano kutatuliwa - Samia Hassan

Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan, amewahimiza wananchi kudumisha na kuuenzi Muungano wa Taganyika na Zanzibar na kuwahakikishia wananchi wa pande hizo mbili kuwa kero chache za Muungano zilizobakia zitamalizwa kwa mazungumzo
Mh. Samia ametoa kauli hiyo kwa nyakati tofauti katika mahojiano na vyombo mbalimbali vya habari katika kuelekea katika Kilele cha Maadhimisho ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambapo sherehe za kitaifa mwaka huu kwa mara ya Kwanza zitafanyika Mjini Dodoma.
Amesisitiza kuwa, tangu Muungano huo uasisiwe umekuwa na manufaa makubwa kwa pande zote mbili kwani jamii zimefahamiana na kushirikiano vizuri katika shughuli za kiuchumi na za kimaendeleo hasa uimarishaji wa ulinzi na usalama kwa wananchi wa pande mbili.
Aidha, amesema, hatua zinazochukuliwa za kutatua kero za Muungano kwa haraka ni jambo jema na la msingi kwani linalenga kuhakikisha Muungano ambao umefikisha miaka 53 sasa unakuwa ni Muungano wa mfano wa kuigwa Duniani.
Kuhusu elimu ya Muungano wa vijana, Makamu wa Rais amesema upo umuhimu mkubwa kwa taasisi za kiserikali za pande mbili kuweka mikakati mizuri ya kuelimisha vijana wa sasa kujua umuhimu wa Muungano ili waweze kuuelewa na kuudumisha.
Mh. Samia amesema kwa sasa vijana wengi wanafuatilia sana mitandao ya kijamii hivyo ni muhimu kwa taasisi za kiserikali zinazoshughulia Muungano kuweka utaratibu wa kupeleka ujumbe mbalimbali kuhusu Muungano kwa jamii hasa vijana kwa ajili ya kuwaelimisha faida za Muungano.
Makamu wa Rais pia amehimiza makundi mbalimbali ya kijamii wakiwemo viongozi wastaafu nchini waendelee na jitihada zao katika kuelimisha umma ili kuuelewa vizuri Muungano kwa ajili ya faida ya jamii nzima na ya Taifa kwa ujumla.

Kupima Malaria sasa ni bure - Waziri Ummy Mwalimu


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Ummy Mwalimu
Serikali ya Tanzania imepiga marufuku vituo vya Umma kuwalipisha wananchi wanaokwenda kupima maambukizi ya ugonjwa wa Malaria kwa kipimo cha MRDT na utoaji wa dawa za mseto (ALUU) zinazotumika kutibu ugonjwa huo kuanzia sasa.
Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Malaria duniani mjini Dodoma, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Ummy Mwalimu amesema vipimo hivyo ni bure na pia mgonjwa asilipishwe fedha kwa dawa za mseto.
“Napenda kusisitiza vituo vya umma vinavyotumia vipimo vya MRDT kwa wagonjwa wa malaria, vipimo hivyo ni bure na pia mgonjwa asilipishwe fedha kwa dawa za mseto ama yule anayelazwa kuchomwa sindano ya ugonjwa huo….Waganga wakuu wa mikoa na wilaya, hakikisheni kuanzia sasa mnafuatilia wahudumu wote na watakaokiuka agizo hili watachukuliwa hatua za kisheria mara moja”. Alisema Bi. Ummy
Aidha, Bi. Ummy amewataka wananchi kushirikiana na serikali kuwafichua wahudumu wa Afya ambao watawalipisha fedha pindi watakapo kuwa wanapima huduma ya Malaria kupitia kipimo cha MRDT ama watakapohitajika kupewa dawa ya mseto (ALUU), pia amezionya maabara binafsi ambazo  zimekuwa zikifanya kazi zake kwa kuangalia zaidi fedha badala ya maisha ya mtu kama kuwaambia wana maambukizi ya malaria wakati hawana.
Pamoja na hayo, amesema takwimu kutoka katika vituo vinavyotolea huduma za afya zinaonyesha takribani watu milioni 12 wanaugua ugonjwa huo kwa mwaka ambapo katika tafiti hizo mkoa wa Kagera, Geita na Kigoma ziliweza kuonekana na viwango vikubwa vya maambukizo kwa mwaka 2015 na 2016 huku wajawazito na watoto chini ya miaka mitano kuonekana kuathiriwa zaidi.

Sababu za serikali kumuondoa Mkurugenzi wa UNDP nchini

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imeliagiza Shirika la Umoja wa Mataifa la Programu ya Maendeleo (United Nations Development Programs – UNDP), kwa upande wa Tanzania kumuondoa nchini Mkurugenzi wa Shirika hilo Bi. Awa Dabo.
Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,imesema Serikali ilifikia uamuzi huo kutokana na Bi. Dabo kutokuwa na maelewano mazuri na baadhi ya watumishi wenzake pamoja na menejimenti ya shirika hilo, hivyo kupelekea kuzoretesha utendaji wa shirika hilo nchini na kupunguza kasi ya kuleta maendeleo kwa Watanzania endapo hatua za haraka zisingechukuliwa.
Baada ya kuthibitishiwa kuondoka nchini, Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje imetoa rai kwa UNDP kuwakumbusha watumishi wake kwamba, kipaumbele chao ni kufanya kazi na Serikali ili kufikia malengo yaliyoainishwa kwenye Dira ya Maendeleo ya Mwaka 2025, Mpango wa Maendeleo wa Miaka mitano na Malengo ya Maendeleo Endelevu ambayo yamefafanuliwa katika Agenda ya Mwaka 2030.
Na Emmy Mwaipopo

HAYA NDIYO MAJIBU YA KAMANDA SIRO KUHUSU UVAMIZI WA CHADEMA

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Simon Sirro amezungumzia vurugu zilizotokea hivi karibuni katika mkutano uliotakiwa kufanyike na maeneo ya Mabibo na Chama cha wananchi CUF. Kamanda huyo amesema kuwa suala hilo na wale waliojeruhiwa upelelezi utasema kama hao watu ndiyo waliokuja kuvamia au la.
Kamanda Sirro amezungumza na wanahabari na kusema kuwa, mikutano ya ndani inaruhusiwa hata bila kutoa taarifa Polisi, lakini kwa waliojeruhiwa amedai kuwa upelelezi utaweka wazi mengi zaidi.
“Kuna hili tukio lililotokea tarehe 22 mwezi wa 4, 2017 majira ya saa tano karibu na nusu kwenye hotel moja inaitwa Vina Hotel, hii hotel iko maeneo ya Mabibo kuna wanachama wa Chama cha CUF maana yake Chama kile kina kundi A na kundi B inaonekana kundi A walikuwa wanafanya mkutano wao ndani ya ukumbi kwahiyo baadhi ya watu ambao tunafuatilia wakiwa na magari yapatayo mawili walivamia mkutano huo na wakafanya fujo, kwahiyo kukawa na vurugu kubwa sana na baadhi ya watu wameumia lakini huyu bwana Juma Shaban Nkumbi huyu Mwenyekiti wa CUF wanasema wa Kinondoni alikuwa ameita mkutano kwahiyo kwenye vurugu hizo kuna baadhi ya watu wameumia suala kubwa ni kujua kwa wale waliokuja kuvamia walikuja kufanya nini ni suala la upelelezi kwasababu mtu kaumia kakatwa na kitu chenye ncha kali,” alisema Kamanda Sirro.
“Amefungua jalada lake akieleza kuwa amepigwa mtu fulani na huyo mtu ndo kamjeruhi kwahiyo je, ni wale waliovamia ni jambo la upelelezi kwahiyo upelelezi utatuambia kama ni wao waliovamia, nilikuwa nawaambia pale hata kama wamevamia je kuna uhalali wa kumkata na mapanga? ni suala la upelelezi kwahiyo kimsingi niseme tu kwamba wale waliokamatwa nikutokana na yale malalamiko dhidi yao ambapo watu wameandika maelezo yao wamewatambua wamewataja kwahiyo ndiyo kesi imefunguliwa na hili la wao kutujulisha ni suala ambalo kwa kawaida wanamjulisha OCD,” alifafanua Kamanda Sirro.
“OCD wetu ndiyo anaweza kujua hilo lakini nafikiri katika busara ya kawaida mikutano ya ndani mara nyingi huwa siyo lazima tutoe kibali kwa hiyo unaweza kuta vyama vingine vya siasa au madhehebu mbalimbali wanaweza hata wasitupe taarifa kwasababu ni mikutano ya ndani lakini nafikiri kama walifanya busara zaidi watakuwa walimjulisha OCD kama mkutano wa namna hiyo ulikuwa unaendelea.”

Profesa Chibunda ateuliwa kuwa Makamu Mkuu wa SUA

Waziri Mkuu akamilisha ukaguzi wa sherehe za Muungano


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amefanya ukaguzi wa miundombinu kwa ajili ya sherehe za miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kusema kuwa, maandalizi yake yako pazuri.
Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo Jumatatu mara baada ya kupokea taarifa ya maandalizi na kukagua Uwanja wa Jamhuri ambapo sherehe hizo zitafanyika na uwanja wa Nyerere Square.
“Nimekuja kuangalia maandalizi ya sherehe hizo yamefikia wapi, najua kutakuwa na maonyesho ya kijeshi zikiwemo michezo na burudani kutoka Tanzania Bara za Visiwani,” alisema.
Hata hivyo Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuwakaribisha wakazi kutoka wilaya zote za mkoa wa Dodoma na mikoa ya jirani wafike kwenye maonyesho hayo ambayo kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania yanafanyika mkoani humo.
“Tunatarajia wageni wengi kutoka nje ya mkoa huu wakiwemo viongozi wastaafu wa kitaifa, waheshimiwa mabalozi na wake wa waasisi wa Taifa hili, Mama Maria Nyerere na Mama Fatma Karume. Pia tutawatambulisha rasmi ndugu zetu waliochanganya udongo wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964,” alisema.

Friday, April 21, 2017

Rais Magufuli kupeleka walimu wa Kiswahili Rwanda

Rais wa Tanzania, Dkt. John Magufuli amepokea barua yenye ujumbe kutoka kwa Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame, iliyowasilishwa kwake na Mjumbe Maalum ambaye ni Waziri wa Elimu wa Rwanda Dkt. Musafiri Papias Malimba.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Dkt. Musafiri Papias, Waziri wa Elimu wa Rwanda na Mjumbe maalumu wa Rais Paul Kagame alipokutana naye Ikulu jijini Dar es salaam, Wengine ni Balozi wa Rwanda nchini Mhe. Eugene Kayihura na Afisa Mwandamizi wa Ubalozi Bw. Issa Mugabutsinze
Rais amepokea barua hiyo, Alhamisi Ikulu, kutoka kwa mjumbe maalum akiwa ni waziri wa Elimu Rwanda Dkt Malimba, aliiwasilisha kwa Rais Magufuli.
Taarifa ya Ikulu imeeleza kuwa pamoja na kupokea barua hiyo, Mheshimiwa Rais Magufuli na Dkt Malimba wamezungumzia masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Rwanda ikiwemo katika sekta ya elimu hususan maendeleo ya sayansi na teknolojia.
Aidha, Mhe. Rais Magufuli ameipongeza Rwanda kwa kuamua lugha ya Kiswahili ianze kufundishwa katika shule zake na ameahidi kuwa Tanzania ipo tayari kutoa walimu wa kwenda kufundisha lugha hiyo.

Marehemu Mh. Elly Macha aagwa rasmi

Waziri mkuu Mh. Kassim Majaliwa pamoja na wabunge mbalimbali wameshiriki kuuaga mwili wa aliyekua mbunge wa Viti Maalum (CHADEMA) Dkt Elly Macha, aliyefariki nchini Uingereza alipokuwa akipatiwa matibabu.
Mwili huo umewasili alfajiri leo, katika uwanja wa Mwalimu Nyerere ambapo mapokezi yaliongozwa na Naibu spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Tulia Ackson na kusafirishwa tena mpaka Dodoma ambapo viongozi wa bunge wamepata fursa ya kuuaga Mheshimiwa Macha kwenye viwanja hivyo vya bunge.
Dkt Macha alifariki dunia Machi 31 mwaka huu katika hospitali ya New Cross, Wolverhampton iliyopo nchini Uingereza alipokuwa akipatiwa matibabu.
Aidha Naibu spika, Dk Tulia Ackson amesema Bunge lilipata taarifa za ugonjwa wa marehemu ndani ya miezi mitatu na baadae kupata taarifa juu ya kifo chake na kusema kwamba, licha ya kua na ulemavu, Dkt Macha alipigania haki za walemavu kijasiri na kikamilifu

BUNGENI : Joshua Nassari Akamatwa Akiwa Anataka Kuingia Bungeni na Chupa ya Kilevi Akiwa Amelewa..!!!


Jana  Bungeni Dodoma, Joshua Nasari(Mb) Arumeru Mashariki amekamatwa na Watu wa Usalama akiwa amelewa huku akiwa na chupa akitaka kuingia nayo Bungeni.

Mb Joshua alipoanza kuchangia alisema kuwa kamati iliyoundwa na Bunge wakati ule wa Rais Kikwete, kumchunguza Waziri Mkuu wa wakati huo Edward Lowassa juu ya tuhuma za Richmond haikutenda haki kabisa.

Akijibu tuhuma hizo kwa kujiamini kabisa, Mh. Harrison Mwakyembe alisema yafuatayo:

"Kwanza niwashukuru vijana wa Usalama kwa kutekeleza majukumu yao hasa ya kumshika Mh. Nasari na chupa hiyo ya kilevi, maana angeweza kutapikia bendera ya Taifa hivyo kulidhalilisha Bunge lote kwa ujumla...

Kuhusu Edward Lowassa na tuhuma hiyo ya Richmond hawezi kusafishika kamwe kwa hali yoyote ile...Tumeshawachoka sana na hatuwezi kuwavumilia tena....

Kamati yangu iliwahoji zaidi ya mashahidi 75,huku kabla ya kuhojiwa kwake na kamati hiyo Edward Lowassa alikimbilia kujiuzuru ghafla...Sasa bhasi kama kuna mtu yeyote hapa Bungeni anayejiamini alete hoja ya kurudisha tuhuma hizo za Richmond kuhusu Edward Lowassa tuanze kuijadili upya..

Na siku tukianza kuijadili upya tuhuma hizo, ntamwomba Mh. Rais JPM anipumzishe Uwaziri ili nilishughulikie hili suala kikamilifu.

pm’ akataa waingereza kuitwa-kumsaka-saanane

Waziri Mkuu Majaliwa alitoa msimamo huo jana bungeni wakati akijibu swali la Mbowe ambaye ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni. Mbowe aliitaka serikali kuomba msaada wa Scotland Yard kuchunguza kupotea kwa Sanane. Mbali na tukio hilo, Mbowe alitaka taasisi hiyo pia ichunguze matukio ya utekaji watu na kuuawa kwa askari polisi mara kwa mara katika mkoa wa Pwani. Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Kamishna Robert Boaz aliiambia Nipashe mwezi mmoja uliopita kuwa ofisi yake haikuwa imefanikiwa kupata taarifa za kilichompata Saanane. Sanane alipotea katika mazingira ya kutatanisha Novemba mwaka jana. Majaliwa alisema serikali haiwezi kualika kikosi hicho cha polisi wa malkia wa Uingereza kwa kuwa vyombo vya ulinzi na usalama nchini vina uwezo mkubwa wa kuchunguza matukio ya uhalifu yanayotokea. Aidha, Majaliwa alisema matukio ya utekaji na mauaji ya polisi yaliyotokea vyombo vya ulinzi na usalama bado vinaendelea na uchunguzi na pindi utakapokamilika taarifa itatolewa. Mbowe alisema ni miezi sita sasa imepita tangu kupotea kwa msaidizi wake huyo na hakuna taarifa yoyote ya serikali kuhusu tukio hilo. Alisema hivi sasa taifa lina hofu, Watanzania wana hofu ya kikatiba na pia watu wanapotea ovyo hali inayosababisha hofu zaidi kwa Watanzania. Mbowe alisema Serikali inapaswa kuomba msaada wa kiuchunguzi kama ilivyowahi kufanywa na Kenya alipouawa kiongozi wa juu wa serikali, Robert Auko, katika mazingira ya kutatanisha. Alisema waliomba msaada katika taasisi hiyo ya Uingereza kuja kuchunguza.

MUSIC