Friday, April 21, 2017

pm’ akataa waingereza kuitwa-kumsaka-saanane

Waziri Mkuu Majaliwa alitoa msimamo huo jana bungeni wakati akijibu swali la Mbowe ambaye ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni. Mbowe aliitaka serikali kuomba msaada wa Scotland Yard kuchunguza kupotea kwa Sanane. Mbali na tukio hilo, Mbowe alitaka taasisi hiyo pia ichunguze matukio ya utekaji watu na kuuawa kwa askari polisi mara kwa mara katika mkoa wa Pwani. Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Kamishna Robert Boaz aliiambia Nipashe mwezi mmoja uliopita kuwa ofisi yake haikuwa imefanikiwa kupata taarifa za kilichompata Saanane. Sanane alipotea katika mazingira ya kutatanisha Novemba mwaka jana. Majaliwa alisema serikali haiwezi kualika kikosi hicho cha polisi wa malkia wa Uingereza kwa kuwa vyombo vya ulinzi na usalama nchini vina uwezo mkubwa wa kuchunguza matukio ya uhalifu yanayotokea. Aidha, Majaliwa alisema matukio ya utekaji na mauaji ya polisi yaliyotokea vyombo vya ulinzi na usalama bado vinaendelea na uchunguzi na pindi utakapokamilika taarifa itatolewa. Mbowe alisema ni miezi sita sasa imepita tangu kupotea kwa msaidizi wake huyo na hakuna taarifa yoyote ya serikali kuhusu tukio hilo. Alisema hivi sasa taifa lina hofu, Watanzania wana hofu ya kikatiba na pia watu wanapotea ovyo hali inayosababisha hofu zaidi kwa Watanzania. Mbowe alisema Serikali inapaswa kuomba msaada wa kiuchunguzi kama ilivyowahi kufanywa na Kenya alipouawa kiongozi wa juu wa serikali, Robert Auko, katika mazingira ya kutatanisha. Alisema waliomba msaada katika taasisi hiyo ya Uingereza kuja kuchunguza.

No comments:

MUSIC