Showing posts with label NEWS. Show all posts
Showing posts with label NEWS. Show all posts

Tuesday, October 17, 2017

Muhubiri aliyesema Mugabe atakufa Leo asema Mungu kasogeza tarehe



Wanasema ni bora ukose kingine chochote lakini sio habari zinazoendelea ulimwenguni sasa hivi ikiwemo hii iliyotokea kwa Rais Mugabe huko Zimbabwe.
Kuna Muhubiri anaitwa Philip Mugadza ambae alitabiri siku kadhaa zilizopita kwamba Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe (93) atafariki October 17 2017.
Alisema hicho ni kitu alionyeshwa na Mungu lakini saa kadhaa zilizopita Muhubiri huyo amejitokeza tena hadharani na kusema Mugabe hatokufa tena October 17 kama ilivyopangwa, Mungu ameahirisha mpaka tarehe nyingine.

Philip Mugadza ( picha ya getty images )
Mugadza amenukuliwa akisema “siku tatu zilizopita nimepokea neno kutoka kwa Mungu akisema kifo cha Mugabe kimeahirishwa mpaka tarehe nyingine ambayo haijatajwa, sio kwamba nimekua nikisali ili afe ndio nionekane mkweli bali hili ni neno la Mungu na lazima nilifikishe kama lilivyo
Kwa upande wa Serikali ya Zimbabwe, Waziri wake wa habari alionekana kucheka kuhusu utabiri wa Mugadza na kusema Rais Mugabe mwenyewe ni Mkristo na amekua akimuabudu Mungu, hawezi kuwa na wasiwasi hata kidogo na utabiri unaofanywa na watu.

Harare
Waziri Simon Khaya Moyo amesema Serikali ya Zimbabwe haikupata wasiwasi wowote kwenye utabiri huo na kwamba kazi zimeendelea kama kawaida, itapendeza tu kujua Muhubiri huyo ndio atakufa lini.

HII KALI NYINGINE,NASSARI KUPELEKA USHAHIDI MWINGINE

Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari (Chadema) amewasilisha ushahidi mwingine kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuhusu tuhuma za ununuzi wa madiwani wa Chama hicho.

Madiwani hao nane wa Chadema wamejiuzulu kwa kile walichoeleza kumuunga mkono Rais John Magufuli jambo ambalo Nassari anadai siyo kweli bali walinunuliwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana nje ya ofisi ya Takukuru Upanga jiji ni humo alisema, " huu ni ushahidi wa tatu na kadri upepelezi ukiwa unaendelea nitaleta mwingine, hii ni kama filamu ya Isidingo."

Nassari alisema alitarajia Rais John Magufuli angewachukulia hatua wateule wake wanaohusishwa katika sakata hilo ili kupisha uchunguzi uweze kufanyika kwa uhuru.

"Tunajiuliza kwa nini Rais hawachukulii hatua DED, DAS au DC wote wa Arumeru kwa kutuhumiwa, watupeleke mahakamani na tungeomba suala hili lichukuliwe kwa uzito wake," alisema Nassari

Naye Mbunge wa Ubungo, Saed Kubunea aliyeongozana na Nassari alisema,"Mimi nimeshiriki hususani kihabari kwani nimewashauri hawa kuutoa kwa umma ili jamii ijue ukweli."

"Tunachojiuliza kwa nini rais yupo kimya, kwa nini mawaziri na viongozi waliotuhumiwa Katika sakata la Almas na Tanzanite aliwasimamisha kwa nini hawa hataki," amehoji Kubenea

Tuesday, August 22, 2017

Tundu Lissu akamatwa na polisi




Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA Tundu Lissu amekamatwa na polisi leo wakati akitoka Mahakama ya Kisutu na kupelekwa Central Police jijini Dar es Salaam
Afisa habari wa CHADEMA Tumaini Makene amethibitisha kukamatwa na Tundu Lissu 
"Tumetoka Mahakama ya Kisutu muda huu ambapo Mwanasheria Mkuu wa Chama, Tundu Lissu alikuwa na kesi ya tuhuma za uchochezi (uchochezi one) lakini pia alikuwa ni wakili kwenye kesi inayomkabili Yericko Nyerere hapa hapa Kisutu. 
Wakati gari la Lissu likiwa liko getini tayari kwa kutoka, likawa blocked na nyuma ya gari yake pia likasimama gari jingine likiwa na askari polisi wenye silaha, kisha wengine wakamfuata na kumwambia yuko chini ya ulinzi na atakiwa kwenda Central Police" alisema Tumaini Makene 
Makene aliendelea kusema baada ya hapo polisi hao walimtaka ashuke kwenye gari yake na kuingia kwenye gari ya polisi kwa ajili ya kwenda Central Police 
Tundu Lissu amekamatwa leo tarehe 22 Agosti 2017 zikiwa zimepita siku tatu toka alipotoa taarifa ya ndege ya Tanzania  'Bombadier Dash Q400' kuzuiliwa nchini Canada kutokana na amri ya mahakama.

Wednesday, July 5, 2017

Kauli ya Yanga kuachana na Dida yawastua mashabiki


Kauli iliyotolewa na Kocha wa Makipa wa Yanga, Juma Pondamali kuwa wameachana na kipa wao Deogratius Munish ‘Dida’ imeonyesha kuwashitua mashabiki wengi wa klabu hiyo.

Wengi wamekuwa wakihoji sababu ya Dida kuondoka na wengine wakimtaka kuvuta subira.

Lakini wako mashabiki wa Yanga wamekuwa wakiutaka uongozi wa Yanga kukaa na kumalizana naye vizuri.

Wengine wameshauri kama amepata timu nje aende lakini si hapa Tanzania.

Pondamali alisema Dida aliwaambia hatasaini mkataba na juhudi za kumbembeleza zimekwama.

Hivyo kips African Lyon waliyemsajili, Beno Kakolanya waliyenaye na watasajili kipa mwingine chipukizi.

Magufuli atoa onyo hili kwa Mwalimu mkuu yeyote atakayeruhusu aliyepata mimba kurudi shul

Rais John Magufuli 

Sengerema. Rais John Magufuli amesema mwalimu mkuu atakayeruhusu mwanafunzi aliyejifungua kurudi shuleni kuendelea na masomo katika shule za Serikali, atafukuzwa kazi.

Rais ameyasema hayo leo (Jumanne, Julai 4) alipokuwa akihutubia wananchi wakati akizindua mradi wa maji Sengerema.

“Ni ukweli pia kuwa wanafunzi waliopata mimba hawarudishwi shuleni, kuna ujanja ujanja wa walimu, wanaandika cheti kuwa alikuwa amelazwa,” amesema na kuongeza:

“Nikimuona Headmaster, amerudisha mwanafunzi aliyepata mimba, kwenye shule za Serikali, yule mwalimu anaondoka.”

Rais amehoji: “Wote waliopata mimba wamebakwa?” Alihoji na kuendelea, “wanafanya mambo haya kwenye picha, wakipata mimba kwa namna hiyo arudi shule.”

Ameongeza: “Niwaombe wazazi wawachunge watoto, hizi mimba zinatokana na wazazi wetu ni lazima wazazi tujifunze kulea, tumechagua kueleza ukweli, tuambiane ukweli.”

Polisi wamkamata Halima Mdee nyumbani kwake


Mbunge wa Kawe, Halima Mdee amekamatwa na polisi wanne na kupelekwa Kituo cha Polisi cha Oysterbay saa  moja iliyopita.

Katibu wa Chadema Mkoa wa Dar es Salaam, Henry Kilewo, amezungumza majira ya  saa 12 jioni na kueleza kuwa Mdee amekamatwa akiwa nyumbani kwake Makongo Juu.

 Awali akizungumza na waandishi wa habari leo asubuhi,  Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ali Hapi aliagiza Jeshi la Polisi kumkamata mbunge huyo  kwa madai kuwa amemkashifu Rais John Magufuli.

Kamanda wa Polisi, mkoa wa Kinondoni, Suzan Kaganda amesema amefanya  hivyo kwa amri ya mkuu huyo wa wilaya.

“Wapi kakamatwa? Sisi tunachojua ni kuwa tunatekeleza agizo la DC (mkuu wa wilaya) mengine muulize kamishna wa kanda maalum, nimetimiza,” amesema.

Tuesday, July 4, 2017

Ufaransa Waipa Tanzania Euro 250,000 kwa ajili ya Wakimbizi



Serikali ya Ufaransa imechangia kiasi cha Euro 250,000 kwa shirika la mpango wa chakula duniani, WFP ili wakimbizi nchini Tanzania waweze kupata msaada zaidi wa kifedha.
Msaada huu unadhihirisha mchango wa serikali ya Ufaransa katika kuhakikisha kuna hali ya usalama wa chakula.

Mwezi Desemba mwaka jana, WFP ilianza kusambaza shilingi za kitanzania 20,000 sawa na dola 9 za marekani kila mwezi kwa wakimbizi 10,000 ukiwa ni mpango wa majaribio uliotekelezwa kwa kushirikiana na washirika ikiwemo serikali ya Tanzania na shirika la umoja wa mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR.

Mchango wa Ufaransa unaiwezesha WFP kuendeleza mradhi huu wa kutoa fedha kwa wakimbizi 10,000 kwa kipindi cha miezi miwili zaidi.

Chini ya mradi huu, wakimbizi wanapokea mgao wa mafuta yatokanayo na mimea, unga kwa ajili ya uji, wakati mgao wa mahindi, na chumvi hubadilishwa kwa fedha.
Kabla ya uzinduzi wa utoaji mgao wa fedha, wakimbizi walikuwa wakipokea msaada wa chakula pekee kutoka WFP.

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa hivi karibuni, asilimia 98 ya wakimbizi wanapenda zaidi kupatiwa msaada wa fedha wakati asilimia 83 wamesema zimewasaidia katika kuimarisha matumizi ya chakula na kupata aina mbali mbali za vyakula.

''Matokeo ya mpango huu wa,msaada wa fedha umekua si njia pekee inayopendelewa na wakimbizi zaidi ya msaada wa chakula lakini pia ni njia ambayo inasaidia kukuza uchumi wao,'' amesema Michael Dunford, mwakilishi wa WFP nchini Tanzania.

Miaka ya karibuni,shirika hilo limekua likiongeza kiasi cha msaada linalotoa kwa mtindo wa fedha na vocha.

Asilimia 29 ya wanaonufaika na WFP hupokea msaada wa chakula kwa njia ya fedha.


Tangu kutokee hali ya kutetereka kwa usalama nchini Burundi mwaka 2015, zaidi ya raia 250,000 wa nchi hiyo walitafuta hifadhi nchini Tanzania, ambayo sasa imewapa makazi wakimbizi 315,000, wengi wao kutoka Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Ifikapo mwishoni mwa mwaka, WFP ina mpango wa kuongeza mgao wa fedha kwa wakimbizi 80,000, shirika linahitaji dola za marekani milioni 6.8 kwa mwezi kuendelea na mpango wa kutoa fedha na chakula kwa wakimbizi nchini Tanzania.

Wednesday, May 10, 2017

Bosi Lucky Vincent kupelekwa mahakamani


Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha ( RPC ), Charles Mkumbo
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha ( RPC ), Charles Mkumbo amesema wanamshikilia mmiliki wa basi dogo aina ya Coaster ambayo ilipata ajali na kusababisha vifo kwa wanafunzi, walimu na dereva siku ya Jumamosi huko Karatu, Arusha.
RPC Mkumbo amedai wanamshikilia mmiliki wa shule hiyo kwa kuruhusu gari yake hiyo kubeba abiria wengi zaidi kuliko uwezo wa gari 
"Siku ya tukio walikuwepo abiria 38 kwenye gari katika uchunguzi baada ya kubaini hilo tumeshachukua hatua kwa mtu aliyewezesha gari hilo kupakia hao watu, tumeshamkamata mmiliki wa gari ambaye ndiye mwenye shule hii, sasa hivi tunaendelea na uchunguzi na utakapokamilika atafikishwa mahakamani" alisema RPC wa Arusha 
Kwa mujibu wa Mkumbo anasema gari hiyo ilikuwa na kibali cha kubeba watu 30 lakini gari hiyo siku ya ajali ilikuwa na watu zaidi ya 30. 

'Grotesque actions' in Penn State fraternity hazing death

Timothy Piazza (c) is seen in this undated photo.Image copyrightABC
Image captionFraternity members waited 12 hours before calling police to help Timothy Piazza (C)
The lawyer for the family of a student who died after falling down stairs during a fraternity initiation has called the group's actions "grotesque".
Timothy Piazza, 19, died in February after he became drunk during a "pledge" event for a fraternity, which is a social club for male students.
Mr Piazza, who was left unconscious for hours, suffered internal injuries before he died in hospital.
Prosecutors charged 18 students at Penn State University over his death.
The charges came after months of a grand jury investigation, which included video from surveillance cameras, testimony and phone records from Mr Piazza's final hours inside the fraternity house.
The report concluded that there was an attempt to conceal evidence of hazing - the initiation ceremony - and underage drinking after Mr Piazza was in hospital.

Syria war: US to arm Kurds in battle for Raqqa

A member of the US-backed Syrian Democratic Forces monitors the town of Tabqa, on April 30, 2017Image copyrightGETTY IMAGES
Image captionThe SDF is pressing IS back in the key city of Tabqa
US President Donald Trump has approved supplying weapons to Kurdish forces fighting so-called Islamic State (IS) in Syria, the Pentagon says.
Kurdish elements of the Syrian Democratic Forces (SDF) would be equipped to help drive IS from its stronghold, Raqqa, a spokeswoman said.
The US was "keenly aware" of Turkey's concerns about such a move, she added.
Turkey views the Kurdish rebels as terrorists and wants to stop them taking more territory in Syria.
The SDF, which comprises Kurdish and Arab militias, is already being supported by elite US forces and air strikes from a US-led coalition.
The group is currently battling IS for control of the city of Tabqa, an IS command centre just 50km (30 miles) from Raqqa.
A Pentagon source told the BBC the equipment would include ammunition, small arms, machine guns, heavy machine guns, construction equipment such as bulldozers and armoured vehicles.
The source added that the US would "seek to recover" the equipment afterwards.

Analysis: Gary O'Donoghue, BBC News, Washington

The US believes the Kurdish fighters - known as the YPG - will be essential to the city's downfall.
The Pentagon sees them as the most disciplined and organised of the anti-IS groups but Turkish opposition has meant Washington has had to tread a fine line.
The imminence of the fight for Raqqa means delay is no longer an option and the Kurds will be getting a range of equipment.
US sources say they have received assurances from the Kurds that they will leave Raqqa to be governed by Syrian Arabs after the battle.
Turkey's President Erdogan is due in Washington next week - he will not be a happy visitor.

No timeline has been given for when the weapons would start to be supplied.
"We are keenly aware of the security concerns of our coalition partner Turkey," said Pentagon spokeswoman Dana White, who is travelling with US Defence Secretary Jim Mattis in Lithuania.
"We want to reassure the people and government of Turkey that the US is committed to preventing additional security risks and protecting our Nato ally."
Turkey sees the Syrian Kurds as an extension of the PKK separatist group inside Turkey which has been designated a terrorist organisation by the US and EU.

Monday, May 8, 2017

Serikali yagharamia msiba wa Arusha


Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania imegharamia Sanda pamoja na majeneza kwa ajili ya Wanafunzi wa Shule ya Lucky Vicent waliopoteza maisha mapema jana kwenye ajali iliyokuwa ikihusisha safari ya kimasomo.
Akitoa taarifa hiyo leo Meya wa Jiji la Arusha , Mh. Calist Lazaro amesema kuwa taarifa za awali zinaonyesha kuwa tayari Serikali imekwishalipia gharama za majeneza na sanda ya kuhifadhia miili ya marehemu ambao kesho wanatarajiwa kufanyiwa ibada katika Uwanja wa mpira wa Sheikh Amri Abeid.
Aidha, Mh. Lazaro amesema kuwa viongozi mbali mbali wakiwemo mawaziri pamoja na wabunge bado wanaendelea kukusanyika katika eneo la shule ya Lucky Vicent  kwa ajili ya kikao na baadae majira ya saa tisa au kumi taarifa rasmi ya serikali itatolewa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha.

Wizi wa Punda tishio Kenya, ngozi yake ndio kitu pekee Wezi wanachukua

CITIZEN TV ya Kenya imeripoti taarifa ya wizi wa punda uliokithiri huko Turkana kiasi kwamba hata Wakazi wenyewe wamejawa na hofu na kisa kikiwa ni kuuzwa kwa ngozi ya punda hao.
Biashara ya kuuzwa ngozi ya punda inadaiwa kuwa imeletwa na Wachina na kufanya ngozi ya mnyama huyo kupanda thamani hadi shilingi za Kenya 10,000 ambazo ni zaidi ya shilingi laki mbili za Tanzania huku Punda mwenyewe akiuzwa Ksh 5000 (laki moja na elfu nane ya Tanzania).
Wanasema baada ya Wachina kuinunua ngozi hiyo husafirishwa na kwenda kutumika kwenye kutengeneza dawa inayotibu magonjwa mbalimbali kwenye mwili wa binadamu.
...>>>”Unaweza nunua punda kwa elfu 5 au sita na ukauza ngozi kwa Elfu 10 hali hiyo ikaleta thamani ya Punda na ndiomaana wezi wanaiba Punda na kumchuna ngozi ili aje auze ngozi peke yake” – Joseph Losuru 
“Tuliona kwenye media za Nigeria kuwa Punda wameisha lakina na hapa kwetu pia Punda wameanza kuisha” – Lokwale Anton Mfugaji

Monday, May 1, 2017

Nape Nnauye amkumbuka Mwalimu Nyerere

Mbunge wa jimbo la Mtama, Mh Nape Nnauye amemkumbuka marehemu baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kuamua kutumia maneno yake katika kufikisha ujumbe wake kwa wananchi kupitia ukurasa wake wa twitter 
Mhe Nape Nnauye alikuwa akitoa ujumbe kuwa maana ya ubinadamu na heshima ya binadamu ni kutokaa kimya pale jambo la uovu linapokuwa likitokea, akiwataka wananchi kutokaa kimya wanapoona kuna jambo la uovu linatendeka.
Ili kufikisha ujumbe huo vizuri Mhe. Nape Nnauye ilibidi atumie clip ya video ya marehemu baba wa taifa, Julius Kambarage Nyerere wakati akihotubia kwa mara ya mwisho katika Mkutano Mkuu. Ambapo mwalimu alisema maneno haya kwa lugha ya kiingerza  
"Hotuba yangu ya mwisho kwenye huu mkutano mkuu, nimeelezea matukio na mienendo na mahitaji kwa namna ambavyo sisi Watanzania tuonavyo, kukaa kimya pale tuonapo hatari, kutulia tu pale tuonapo sera hatari ambazo ziko kinyume na kulinda amani na haki, kufanya hivyo itakuwa tunaachia uhuru wetu na utu wetu kamwe hatutafanya hivyo" Mwalimu Nyerere 
Baada ya kuweka video hiyo ya Mwalimu Nyerere Nape Nnauye naye aliweka ujumbe wake ambao ulisomeka hivi 
"Heshima ya binadamu na maana ya kweli ya ubinadamu ni kutokaa kimya pale uovu unapotendeka" aliandika Nape Nnauye   

Rais Magufuli atoa onyo kwa makampuni ya simu nchini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli ametahadharisha kuwa, wapo mbioni kuhakikisha mapato ya serikali yanadhibitiwa zaidi ili taifa liweze kujitegemea kikamilifu, huku akionya makampuni ya simu nchini.
Rais Magufuli ameyasema hayo Ijumaa hii, mjini Dodoma wakati akikabidhiwa taarifa ya vyeti feki. Rais ameyaonya makampuni hayo, akisema, dawa ya makampuni hayo bado inatengenezwa.
“Bado kuna maeneo mengi ambayo tunaibiwa fedha. Kwenye haya makampuni ya simu haya, yanafanya transactions nyingi lakini hela haziingii serikalini, dawa yao tunaitengeneza baada ya muda mfupi kidogo itakamilika,” alisema Rais Magufuli huku akishangiliwa.

Friday, April 28, 2017

Bashe aishukia serikali ya Kenya

Mbunge wa Nzega mjini, Hussein Bashe amesikitishwa na Serikali ya Kenya kuweka zuio la kuingiza mitungi ya gesi inayotoka Tanzania na kusema ni vizuri nchi hiyo ikaheshimu mikataba ya ‘East African Community (EAC) .
Mbunge huyo ameandika hayo kupitia ukurasa wake Twitter hivi:
Quality ,Dar port and Cost ya Gesi inayotoka Tz ndo competitive edge ya Ma kampuni ya Tz dhidi ya Yale ya kenya uamuzi huu si sawa.
Serekali ya Kenya imezuia Gesi za matumizi ya nyumbani zinazotoka Tz kuingia Kenya ni vizuri Kenya ikaheshimu EAC treaty “Common mkt”
Bashe amesema hayo baada ya serikali ya Kenya, kupitia Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Andrew Kamau kupiga marufuku uagizaji wa gesi ya kupikia kutoka Tanzania kupitia mipaka ya nchi hiyo.

Meli ya kijasusi ya Urusi yazama Uturuki

Meli ya Liman ikipitia mlango wa bahari wa Bosphorus mwezi OktobaHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMeli ya Liman ikipitia mlango wa bahari wa Bosphorus mwezi Oktoba
Meli ya kijasusi ya Urusi imezama baharini katika pwani ya Uturuki baada ya kugongana na meli ya kubeba mizigo, maafisa wa uchukuzi wa baharini wa Uturuki wamesema.
Wote waliokuwa kwenye meli hiyo wameokolewa.
Urusi awali ilikuwa imethibitisha kwamba meli ya Liman, ambayo ni sehemu ya kundi la meli za taifa hilo katika Bahari Nyeusi ilikuwa imepatwa na hitilafu na kwamba juhudi za kuizuia kuzama zilikuwa zinaendelea.
Chanzo cha kugongana kwa meli hizo hakijabainika lakini kulikuwa na ukungu mwingi eneo hilo.
Meli hiyo ya kijasusi iligonga meli yenye bendera ya Togo ambayo ilikuwa ikisafirisha mizigo, vyombo vya habari Uturuki vinasema.
Waziri mkuu wa Uturuki Binali Yildirim amezungumza na mwenzake wa Urusi Dmitry Medvedev, na kumueleza masikitiko na huzuni yake kutokana na ajali hiyo, duru katika afisi ya waziri mkuu huyo wa Uturuki zimenukuliwa na shirika la habari la Reuters.
Kundi la Meli za Urusi Bahari Nyeusi (BSF) hupitia mlango wa bahari wa Bosphorus Strait kuelekea bahari ya Mediterranean, ambapo hushiriki katika harakati za kijeshi Syria.
Meli hiyo ya Urusi ilikuwa na watu 78 ambao waliokolewa wote.
Ramani
Meli hiyo iligongana na meli ya Youzarsif H takriban 29km kutoka mji wa Kilyos kaskazini mwa mji wa Istanbul.
Haijabainika iwapo meli hiyo ilikuwa inaelekea mlango wa bahari wa Bosphorus wakati huo.

Venezuela kujiondoa kwenye umoja wa OAS

Nchi ya Venezuela imetangaza kujiondoa katika shirika la umoja wa mataifa ya Marekani Kusini (OAS ) kwa madai kuwa, nchi zilizopo ndani ya jumuiya hiyo zinaingilia masuala ya ndani ya nchi yao.
Akiongea na kituo cha runinga cha taifa (VTV), Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo, Delcy Rodriguez amesema, “Katika OAS, tulitangaza kwamba hatua hizi za usumbufu, zimeegemea upande mmoja, haramu.Tutachukua hatua za haraka za kuandaa barua kwa OAS na kuelezea ni ya kujiondoa kwa Venezuela kwenye huu umoja.”
“Kesho, kama alivyotaka Rais Nicolas Maduro, tutawasilisha barua ya kujiondoa katika umoja wa OAS na tutaanza hatua hizo ambazo zitachukua miezi 24,” ameongeza.
Watu wapatao 30 wamefariki dunia katika maandamano yanayoendelea nchini humo kwa takribani wiki ya tatu sasa,wakimtaka rais Nicolas Maduro kujiuzulu kutokana kuzorota kwa uchumi wa nchi hiyo jambo lililosababisha upungufu mkubwa wa chakula.

MUSIC