Friday, April 28, 2017

US: Mfumo wa kujilinda ''utamuamsha'' rais wa K. Kaskazini

Upelekaji wa mfumo wa kujilinda dhidi ya makombora nchini Korea Kusini ulipingwa na waandamanajiHaki miliki ya pichaAFP
Image captionUpelekaji wa mfumo wa kujilinda dhidi ya makombora nchini Korea Kusini ulipingwa na waandamanaji
Mfumo wa kujilinda dhidi ya makombora wa Marekani unaowekwa nchini Korea Kusini utaanza kufanya kazi katika siku chache zijazo, jeshi la Marekani limesema.
Mfumo huo wa Thaad umetengezwa kuilinda Korea Kusini na majeshi ya Marekani yaliopiga kambi nchini humo dhidi ya vitisho vya Korea Kaskazini.
Vifaa vya mfumo huo vilipelekwa katika taifa hilo siku ya Jumatano, Admirali Harry Harris ambaye ni ni kamanda wa eneo la Pacific alisema kuwa Thaada itaanza kufanya kazi katika siku chache zijazo ili kuiinda Korea Kusini dhidi ya vitisho vya jirani yake Korea kaskazini.

No comments:

MUSIC