Saturday, May 4, 2024
Saturday, April 20, 2024
Sunday, April 14, 2024
ALLY KAMWE ATAMBA NA GUEDE,AHMED ALLY ATIA MBWEMBWE KUIFUNGA YANGA
ALLY KAMWE: ATAMBA NA AZIZ KI NA GUEDE BAADA YA USHINDI | AGUSIA DABI | NBCPL: SINGIDA FG 0-3 YANGA
AHMED ALLY: HATUWEZI KUKUBALI KUFUNGWA MARA MBILI NA TIMU MOJA/YANGA WANAJIAMINI SANA
Saturday, April 13, 2024
MAZOEZI YA YANGA TISHIO , AHMED ALLY KILIO TUPU DHIDI YA IHEFU
MAZOEZI YA MWISHO KABLA YA KUMKANDA SINGIDA KESHO
Thursday, April 11, 2024
Tuesday, October 17, 2017
Muhubiri aliyesema Mugabe atakufa Leo asema Mungu kasogeza tarehe
Wanasema ni bora ukose kingine chochote lakini sio habari zinazoendelea ulimwenguni sasa hivi ikiwemo hii iliyotokea kwa Rais Mugabe huko Zimbabwe.
Kuna Muhubiri anaitwa Philip Mugadza ambae alitabiri siku kadhaa zilizopita kwamba Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe (93) atafariki October 17 2017.
Alisema hicho ni kitu alionyeshwa na Mungu lakini saa kadhaa zilizopita Muhubiri huyo amejitokeza tena hadharani na kusema Mugabe hatokufa tena October 17 kama ilivyopangwa, Mungu ameahirisha mpaka tarehe nyingine.
Philip Mugadza ( picha ya getty images )
Mugadza amenukuliwa akisema “siku tatu zilizopita nimepokea neno kutoka kwa Mungu akisema kifo cha Mugabe kimeahirishwa mpaka tarehe nyingine ambayo haijatajwa, sio kwamba nimekua nikisali ili afe ndio nionekane mkweli bali hili ni neno la Mungu na lazima nilifikishe kama lilivyo“
Kwa upande wa Serikali ya Zimbabwe, Waziri wake wa habari alionekana kucheka kuhusu utabiri wa Mugadza na kusema Rais Mugabe mwenyewe ni Mkristo na amekua akimuabudu Mungu, hawezi kuwa na wasiwasi hata kidogo na utabiri unaofanywa na watu.
Harare
Waziri Simon Khaya Moyo amesema Serikali ya Zimbabwe haikupata wasiwasi wowote kwenye utabiri huo na kwamba kazi zimeendelea kama kawaida, itapendeza tu kujua Muhubiri huyo ndio atakufa lini.
ZARI THE BOSS ,AMWAGA CHOZI KWA JAMAA
Kwa wewe unaefatilia habari za mastaa wa bongo na hasa uhusiano wa Mwimbaji Diamond Platnumz na Zari hivi karibuni utakua umeona meeengi yameandikwa na hata Diamond mwenyewe kukiri kuhusu mtafaruku ulioukumba uhusiano huo.
Wengi waliamini kwamba huu ndio unaweza ukawa mwisho wa wawili hawa hasa Zari ambae alionekana kukasirika zaidi baada ya Diamond kukiri kuzaa na Hamisa Mobetto ambapo Zari alifuta picha zote za Diamond pamoja na kutoa kauli zisizopungua 5 zikionyesha dalili za kumalizana na D.
Hata hivyo upepo unaonekana kubadilika baada ya Zari kuanza kuonekana taratibu akiwa na dalili za kurejesha mapenzi yake kwa Diamond Platnumz.
Diamond alipost wimbo mpya wa Harmonize na kutumia mistari hiyo kama dedication kwa Zari ambapo aliandika >>> “We Hodari Mtunza Siri Zangu Hata nikiwa Sina… Hunivumilia na kuamini nitapata… Tafadhali nlindie Roho yangu cha Kukupa sina ila nakuapia Hakiamungu sito kuacha….) Ujumbe wako huo mama
@zarithebosslady #SHULALA“
Baada ya hiyo Zari nae alishukuru na kuweka emoji ya kutokwa chozi kutokana na maneno mazito aliyoyaandika Diamond.
HUYU AMETISHA ,MABOMU ASAFIRISHA KWENYE MADUMU

Askari walimshtukia kijana huyo baada ya kupita kwenye vituo vitatu bila kusimama huku gari hilo likielekea kwenye kambi ya majeshi ya Umoja wa Mataifa kwa spidi kali.
Polisi mjini Kabul wamesema walitumia nguvu kubwa kumsimamisha kwa kulishambulia gari lake kwa risasi.
Wanajeshi wa UN nchini humo wamesema kuwa mabomu hayo yalichanganywa na mbolea na kuwekwa kwenye madumu huku mengine yakiwa kwenye maboksi ya nyanya hii ni baada ya kufanyiwa ukaguzi.
Hata hivyo, mpaka sasa hakuna kundi lolote la kigaidi lilitoa tamko juu ya tukio hilo.
Kwa mujibu wa UN nchini Afghanistan mamia ya raia wanauawa kila mwezi na makundi ya kigaidi ambapo kuanzia mwezi Januari hadi Septemba watu 1,584 wameshauawa kwenye matukio mbalimbali ya mashambulizi ya kigaidi.
HII KALI NYINGINE,NASSARI KUPELEKA USHAHIDI MWINGINE
Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari (Chadema) amewasilisha ushahidi mwingine kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuhusu tuhuma za ununuzi wa madiwani wa Chama hicho.
Madiwani hao nane wa Chadema wamejiuzulu kwa kile walichoeleza kumuunga mkono Rais John Magufuli jambo ambalo Nassari anadai siyo kweli bali walinunuliwa.
Akizungumza na waandishi wa habari jana nje ya ofisi ya Takukuru Upanga jiji ni humo alisema, " huu ni ushahidi wa tatu na kadri upepelezi ukiwa unaendelea nitaleta mwingine, hii ni kama filamu ya Isidingo."
Nassari alisema alitarajia Rais John Magufuli angewachukulia hatua wateule wake wanaohusishwa katika sakata hilo ili kupisha uchunguzi uweze kufanyika kwa uhuru.
"Tunajiuliza kwa nini Rais hawachukulii hatua DED, DAS au DC wote wa Arumeru kwa kutuhumiwa, watupeleke mahakamani na tungeomba suala hili lichukuliwe kwa uzito wake," alisema Nassari
Naye Mbunge wa Ubungo, Saed Kubunea aliyeongozana na Nassari alisema,"Mimi nimeshiriki hususani kihabari kwani nimewashauri hawa kuutoa kwa umma ili jamii ijue ukweli."
"Tunachojiuliza kwa nini rais yupo kimya, kwa nini mawaziri na viongozi waliotuhumiwa Katika sakata la Almas na Tanzanite aliwasimamisha kwa nini hawa hataki," amehoji Kubenea
Tuesday, August 22, 2017
Tundu Lissu akamatwa na polisi
Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA Tundu Lissu amekamatwa na polisi leo wakati akitoka Mahakama ya Kisutu na kupelekwa Central Police jijini Dar es Salaam
Afisa habari wa CHADEMA Tumaini Makene amethibitisha kukamatwa na Tundu Lissu
"Tumetoka Mahakama ya Kisutu muda huu ambapo Mwanasheria Mkuu wa Chama, Tundu Lissu alikuwa na kesi ya tuhuma za uchochezi (uchochezi one) lakini pia alikuwa ni wakili kwenye kesi inayomkabili Yericko Nyerere hapa hapa Kisutu.
Wakati gari la Lissu likiwa liko getini tayari kwa kutoka, likawa blocked na nyuma ya gari yake pia likasimama gari jingine likiwa na askari polisi wenye silaha, kisha wengine wakamfuata na kumwambia yuko chini ya ulinzi na atakiwa kwenda Central Police" alisema Tumaini Makene
Makene aliendelea kusema baada ya hapo polisi hao walimtaka ashuke kwenye gari yake na kuingia kwenye gari ya polisi kwa ajili ya kwenda Central Police
Tundu Lissu amekamatwa leo tarehe 22 Agosti 2017 zikiwa zimepita siku tatu toka alipotoa taarifa ya ndege ya Tanzania 'Bombadier Dash Q400' kuzuiliwa nchini Canada kutokana na amri ya mahakama.
Emmanuel Okwi aiogopa Yanga
Mshambuliaji wa kimataifa wa Simba, raia wa Uganda, Emmanuel Okwi amefunguka kwa kujitapa kuwa kuelekea mechi dhidi ya watani wa jadi 'Ngao ya Hisani' kesho atahakikisha anaifunga Yanga japo amepatwa na kitete cha kusema ni magoli mangapi ataifunga.
Okwi ameeleza hayo kupitia mahojiano maalum aliyofanya na klabu yake na kusema hawezi kusema ni magoli mangapi atawapachika 'gongo wazi' Yanga kwa kuwa ni klabu ambayo anaiheshimu.
"Game ya Yanga siku zote haiwagi rahisi kwa upande wowote kwa kuwa ni timu yenye wachezaji wazoefu wengi japo na sisi tunawachezaji wazoefu wengi kama wao, tunategemea mchezo wa kesho utakuwa mzuri pia tunamatumaini tutashinda", alisema Okwi.
Pamoja na hayo, Okwi aliendelea kwa kusema "nitahakikisha timu yangu inashirikiana vizuri na wachezaji wenzangu ili tuweze kutoka na matokeo mazuri katika mchezo huo. Siwezi kusema tutawafunga magoli mangapi kwa kuwa ni timu ambayo ninaiheshimu lakini sisi tutajipanga kuhakikisha tunatoka na matokeo mazuri", alisisitiza Okwi.
Okwi ameanza tambwe hizo ikiwa imebakia siku moja kuchezwa kwa mechi ya watani wa jadi siku ya kesho (Jumatano) ambapo mchezo huo umekuwa ukisubiliwa na watu mbalimbali waweze kujua ni nani siku hiyo ataweza kumfunika mwenzake.
Wednesday, July 5, 2017
Kauli ya Yanga kuachana na Dida yawastua mashabiki
Kauli iliyotolewa na Kocha wa Makipa wa Yanga, Juma Pondamali kuwa wameachana na kipa wao Deogratius Munish ‘Dida’ imeonyesha kuwashitua mashabiki wengi wa klabu hiyo.
Wengi wamekuwa wakihoji sababu ya Dida kuondoka na wengine wakimtaka kuvuta subira.
Lakini wako mashabiki wa Yanga wamekuwa wakiutaka uongozi wa Yanga kukaa na kumalizana naye vizuri.
Wengine wameshauri kama amepata timu nje aende lakini si hapa Tanzania.
Pondamali alisema Dida aliwaambia hatasaini mkataba na juhudi za kumbembeleza zimekwama.
Hivyo kips African Lyon waliyemsajili, Beno Kakolanya waliyenaye na watasajili kipa mwingine chipukizi.
Magufuli atoa onyo hili kwa Mwalimu mkuu yeyote atakayeruhusu aliyepata mimba kurudi shul
Rais John Magufuli
Sengerema. Rais John Magufuli amesema mwalimu mkuu atakayeruhusu mwanafunzi aliyejifungua kurudi shuleni kuendelea na masomo katika shule za Serikali, atafukuzwa kazi.
Rais ameyasema hayo leo (Jumanne, Julai 4) alipokuwa akihutubia wananchi wakati akizindua mradi wa maji Sengerema.
“Ni ukweli pia kuwa wanafunzi waliopata mimba hawarudishwi shuleni, kuna ujanja ujanja wa walimu, wanaandika cheti kuwa alikuwa amelazwa,” amesema na kuongeza:
“Nikimuona Headmaster, amerudisha mwanafunzi aliyepata mimba, kwenye shule za Serikali, yule mwalimu anaondoka.”
Rais amehoji: “Wote waliopata mimba wamebakwa?” Alihoji na kuendelea, “wanafanya mambo haya kwenye picha, wakipata mimba kwa namna hiyo arudi shule.”
Ameongeza: “Niwaombe wazazi wawachunge watoto, hizi mimba zinatokana na wazazi wetu ni lazima wazazi tujifunze kulea, tumechagua kueleza ukweli, tuambiane ukweli.”
Zambia yaikamia Taifa Stars Cosafa
Afrika Kusini. Timu ya Zambia inashuka dimbani kesho Jumatano kukabiliana na Taifa Stars kwenye mchezo wa nusu fainali unaotarajiwa kuwa na ushindani mkali.
Mchezo huo utapigwa mjini Rustenburg, Afrika Kusini huku Kocha Wedson Nyirenda akisisitiza kuwa, kikosi chake cha Chipolopolo kina matumaini ya kuibuka na ushindi.
Katika mechi mbili kabla ya mashindano hayo, timu hiyo hiyo ilipoteza mchezo mbele ya Msumbiji kwa kufungwa bao 1-0 wakati wa mechi ya kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) na nyingine ikaifunga Afrika Kusini kwenye mechi ya kirafiki.
Hata hivyo, katika mashindano ya Cosafa walishinda mabao 2- 1 dhidi ya Botswana mchezo uliopigwa juzi Jumapili.
Zambia watashuka Uwanjani wakimtegemea mshambuliajia wao, Donashano Malama.
Mchezo huo utapigwa mjini Rustenburg, Afrika Kusini huku Kocha Wedson Nyirenda akisisitiza kuwa, kikosi chake cha Chipolopolo kina matumaini ya kuibuka na ushindi.
Katika mechi mbili kabla ya mashindano hayo, timu hiyo hiyo ilipoteza mchezo mbele ya Msumbiji kwa kufungwa bao 1-0 wakati wa mechi ya kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) na nyingine ikaifunga Afrika Kusini kwenye mechi ya kirafiki.
Hata hivyo, katika mashindano ya Cosafa walishinda mabao 2- 1 dhidi ya Botswana mchezo uliopigwa juzi Jumapili.
Zambia watashuka Uwanjani wakimtegemea mshambuliajia wao, Donashano Malama.
Polisi wamkamata Halima Mdee nyumbani kwake
Mbunge wa Kawe, Halima Mdee amekamatwa na polisi wanne na kupelekwa Kituo cha Polisi cha Oysterbay saa moja iliyopita.
Katibu wa Chadema Mkoa wa Dar es Salaam, Henry Kilewo, amezungumza majira ya saa 12 jioni na kueleza kuwa Mdee amekamatwa akiwa nyumbani kwake Makongo Juu.
Awali akizungumza na waandishi wa habari leo asubuhi, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ali Hapi aliagiza Jeshi la Polisi kumkamata mbunge huyo kwa madai kuwa amemkashifu Rais John Magufuli.
Kamanda wa Polisi, mkoa wa Kinondoni, Suzan Kaganda amesema amefanya hivyo kwa amri ya mkuu huyo wa wilaya.
“Wapi kakamatwa? Sisi tunachojua ni kuwa tunatekeleza agizo la DC (mkuu wa wilaya) mengine muulize kamishna wa kanda maalum, nimetimiza,” amesema.
Subscribe to:
Comments (Atom)




