Wednesday, July 5, 2017

Kauli ya Yanga kuachana na Dida yawastua mashabiki


Kauli iliyotolewa na Kocha wa Makipa wa Yanga, Juma Pondamali kuwa wameachana na kipa wao Deogratius Munish ‘Dida’ imeonyesha kuwashitua mashabiki wengi wa klabu hiyo.

Wengi wamekuwa wakihoji sababu ya Dida kuondoka na wengine wakimtaka kuvuta subira.

Lakini wako mashabiki wa Yanga wamekuwa wakiutaka uongozi wa Yanga kukaa na kumalizana naye vizuri.

Wengine wameshauri kama amepata timu nje aende lakini si hapa Tanzania.

Pondamali alisema Dida aliwaambia hatasaini mkataba na juhudi za kumbembeleza zimekwama.

Hivyo kips African Lyon waliyemsajili, Beno Kakolanya waliyenaye na watasajili kipa mwingine chipukizi.

Magufuli atoa onyo hili kwa Mwalimu mkuu yeyote atakayeruhusu aliyepata mimba kurudi shul

Rais John Magufuli 

Sengerema. Rais John Magufuli amesema mwalimu mkuu atakayeruhusu mwanafunzi aliyejifungua kurudi shuleni kuendelea na masomo katika shule za Serikali, atafukuzwa kazi.

Rais ameyasema hayo leo (Jumanne, Julai 4) alipokuwa akihutubia wananchi wakati akizindua mradi wa maji Sengerema.

“Ni ukweli pia kuwa wanafunzi waliopata mimba hawarudishwi shuleni, kuna ujanja ujanja wa walimu, wanaandika cheti kuwa alikuwa amelazwa,” amesema na kuongeza:

“Nikimuona Headmaster, amerudisha mwanafunzi aliyepata mimba, kwenye shule za Serikali, yule mwalimu anaondoka.”

Rais amehoji: “Wote waliopata mimba wamebakwa?” Alihoji na kuendelea, “wanafanya mambo haya kwenye picha, wakipata mimba kwa namna hiyo arudi shule.”

Ameongeza: “Niwaombe wazazi wawachunge watoto, hizi mimba zinatokana na wazazi wetu ni lazima wazazi tujifunze kulea, tumechagua kueleza ukweli, tuambiane ukweli.”

Zambia yaikamia Taifa Stars Cosafa

Afrika Kusini. Timu ya Zambia inashuka dimbani kesho Jumatano kukabiliana na Taifa Stars kwenye mchezo wa nusu fainali unaotarajiwa kuwa na ushindani mkali.

Mchezo huo utapigwa mjini Rustenburg, Afrika Kusini huku Kocha Wedson Nyirenda akisisitiza kuwa,  kikosi chake cha Chipolopolo kina matumaini ya kuibuka na ushindi.

Katika mechi mbili kabla ya mashindano hayo, timu hiyo hiyo ilipoteza mchezo mbele ya Msumbiji kwa kufungwa bao 1-0  wakati wa mechi ya kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon)  na nyingine ikaifunga Afrika Kusini kwenye mechi ya kirafiki.

Hata hivyo, katika mashindano ya Cosafa walishinda mabao 2- 1 dhidi ya Botswana mchezo uliopigwa juzi Jumapili.

Zambia watashuka Uwanjani wakimtegemea mshambuliajia wao, Donashano Malama.

Polisi wamkamata Halima Mdee nyumbani kwake


Mbunge wa Kawe, Halima Mdee amekamatwa na polisi wanne na kupelekwa Kituo cha Polisi cha Oysterbay saa  moja iliyopita.

Katibu wa Chadema Mkoa wa Dar es Salaam, Henry Kilewo, amezungumza majira ya  saa 12 jioni na kueleza kuwa Mdee amekamatwa akiwa nyumbani kwake Makongo Juu.

 Awali akizungumza na waandishi wa habari leo asubuhi,  Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ali Hapi aliagiza Jeshi la Polisi kumkamata mbunge huyo  kwa madai kuwa amemkashifu Rais John Magufuli.

Kamanda wa Polisi, mkoa wa Kinondoni, Suzan Kaganda amesema amefanya  hivyo kwa amri ya mkuu huyo wa wilaya.

“Wapi kakamatwa? Sisi tunachojua ni kuwa tunatekeleza agizo la DC (mkuu wa wilaya) mengine muulize kamishna wa kanda maalum, nimetimiza,” amesema.

Tuesday, July 4, 2017

Ufaransa Waipa Tanzania Euro 250,000 kwa ajili ya Wakimbizi



Serikali ya Ufaransa imechangia kiasi cha Euro 250,000 kwa shirika la mpango wa chakula duniani, WFP ili wakimbizi nchini Tanzania waweze kupata msaada zaidi wa kifedha.
Msaada huu unadhihirisha mchango wa serikali ya Ufaransa katika kuhakikisha kuna hali ya usalama wa chakula.

Mwezi Desemba mwaka jana, WFP ilianza kusambaza shilingi za kitanzania 20,000 sawa na dola 9 za marekani kila mwezi kwa wakimbizi 10,000 ukiwa ni mpango wa majaribio uliotekelezwa kwa kushirikiana na washirika ikiwemo serikali ya Tanzania na shirika la umoja wa mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR.

Mchango wa Ufaransa unaiwezesha WFP kuendeleza mradhi huu wa kutoa fedha kwa wakimbizi 10,000 kwa kipindi cha miezi miwili zaidi.

Chini ya mradi huu, wakimbizi wanapokea mgao wa mafuta yatokanayo na mimea, unga kwa ajili ya uji, wakati mgao wa mahindi, na chumvi hubadilishwa kwa fedha.
Kabla ya uzinduzi wa utoaji mgao wa fedha, wakimbizi walikuwa wakipokea msaada wa chakula pekee kutoka WFP.

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa hivi karibuni, asilimia 98 ya wakimbizi wanapenda zaidi kupatiwa msaada wa fedha wakati asilimia 83 wamesema zimewasaidia katika kuimarisha matumizi ya chakula na kupata aina mbali mbali za vyakula.

''Matokeo ya mpango huu wa,msaada wa fedha umekua si njia pekee inayopendelewa na wakimbizi zaidi ya msaada wa chakula lakini pia ni njia ambayo inasaidia kukuza uchumi wao,'' amesema Michael Dunford, mwakilishi wa WFP nchini Tanzania.

Miaka ya karibuni,shirika hilo limekua likiongeza kiasi cha msaada linalotoa kwa mtindo wa fedha na vocha.

Asilimia 29 ya wanaonufaika na WFP hupokea msaada wa chakula kwa njia ya fedha.


Tangu kutokee hali ya kutetereka kwa usalama nchini Burundi mwaka 2015, zaidi ya raia 250,000 wa nchi hiyo walitafuta hifadhi nchini Tanzania, ambayo sasa imewapa makazi wakimbizi 315,000, wengi wao kutoka Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Ifikapo mwishoni mwa mwaka, WFP ina mpango wa kuongeza mgao wa fedha kwa wakimbizi 80,000, shirika linahitaji dola za marekani milioni 6.8 kwa mwezi kuendelea na mpango wa kutoa fedha na chakula kwa wakimbizi nchini Tanzania.

John Bocco aitwa Afrika Kusini kujiunga na Taifa Stars

Mshambuliaji mpya wa Simba, John Raphael Bocco ametua nchini Afrika Kusini kwa ajili ya kujiunga na kikosi cha timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars kilichopo nchini humo kutokana na mchezaji Mbaraka Yusuph kuwa majeruhi.

Hayo yamebainishwa na Kaimu Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Salum Madadi ambapo amesema Bocco ameondoka jana nchini kuwafuata wenzake walioko huko kwa lengo la kuchukua nafasi ya mshambuliaji huyo mpya kutoka Azam Fc.

“Mbaraka amepata matatizo kule Afrika Kusini, hali ya hewa ya baridi imemletea matatizo ambayo kwa sasa yanamzuia kucheza hivyo wakati tunatazama hali yake tumemuita Bocco kwanza kuchukua nafasi,” alisema Madadi.

Taifa Stars itashuka dimbani kwa mara nyingine siku ya Jumatano dhidi ya Zambia katika hatua ya nusu fainali ya michuano ya COSAFA inayoendelea kuchezwa huko Afrika Kusini baada ya kuichakaza bao 1-0 Bafana Bafana usiku wa kuamkia leo.

Rasmi John Terry ajiunga Aston Villa

HATIMAYE baada ya kuambiwa hatoongezewa mkataba na klabu aliyoichezea kwa muda mrefu nahodha wa zamani wa Chelsea na England John Terry amesaini kuichezea klabu ya Aston Villa inayoshiriki Championship licha ya kuwa na umri wa miaka 37.

Mmiliki na Mwenyekiti wa Villa Dr Tony Xia alithibitisha kuwasili kwa staa huyo aliyepata mafanikio makubwa akiwa na Chelsea Jumatatu asubuhi, akiandika kwenye Twitter yake: ‘Karibu JT Birmingham city…Aston Villa! #UTV! @AVFCOfficial!’

Kuwasili kwa Terry ambaye alikuwa anawindwa pia na mahasimu wa Villa, Birmingham City kuliwafanya mashabiki wa klabu hiyo kuanzisha group maalumu la WhatsApp kwa ajili ya kumkarubisha.


Alvaro Morata akaribia kutua Man United

UHAMISHO wa Alvaro Morata kwenda Manchester United unakaribia kukamilika baada ya wakala na baba wa mshambuliaji huyo kuhudhuria kikao cha mazungumzo na Real Madrid Jumatatu.

Taarifa nchini Hispania zimesema kwamba Juanma Lopez na Alfonso Morata walikwenda katika ofisi za Real mida ya mchana kukutana na viongozi.

Kikao hicho kilimalizika baada ya muda wa saa moja kwa mujibu wa AS na thamani ya Morata ambaye anatakiwa sana na Manchester United ni Pauni Milioni 70.

Pamoja na hayo, Mashetani hao Wekundu bado hawajaafiki bei ya manunuzi ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24, ambaye amefunga mabao 20 katuika mechi 43 msimu uliopita. 

Taarifa za kikao baina ya Lopez na Real azinazidi kuongeza uwezekano wa uhamisho huo.

Wednesday, May 10, 2017

Bosi Lucky Vincent kupelekwa mahakamani


Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha ( RPC ), Charles Mkumbo
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha ( RPC ), Charles Mkumbo amesema wanamshikilia mmiliki wa basi dogo aina ya Coaster ambayo ilipata ajali na kusababisha vifo kwa wanafunzi, walimu na dereva siku ya Jumamosi huko Karatu, Arusha.
RPC Mkumbo amedai wanamshikilia mmiliki wa shule hiyo kwa kuruhusu gari yake hiyo kubeba abiria wengi zaidi kuliko uwezo wa gari 
"Siku ya tukio walikuwepo abiria 38 kwenye gari katika uchunguzi baada ya kubaini hilo tumeshachukua hatua kwa mtu aliyewezesha gari hilo kupakia hao watu, tumeshamkamata mmiliki wa gari ambaye ndiye mwenye shule hii, sasa hivi tunaendelea na uchunguzi na utakapokamilika atafikishwa mahakamani" alisema RPC wa Arusha 
Kwa mujibu wa Mkumbo anasema gari hiyo ilikuwa na kibali cha kubeba watu 30 lakini gari hiyo siku ya ajali ilikuwa na watu zaidi ya 30. 

'Grotesque actions' in Penn State fraternity hazing death

Timothy Piazza (c) is seen in this undated photo.Image copyrightABC
Image captionFraternity members waited 12 hours before calling police to help Timothy Piazza (C)
The lawyer for the family of a student who died after falling down stairs during a fraternity initiation has called the group's actions "grotesque".
Timothy Piazza, 19, died in February after he became drunk during a "pledge" event for a fraternity, which is a social club for male students.
Mr Piazza, who was left unconscious for hours, suffered internal injuries before he died in hospital.
Prosecutors charged 18 students at Penn State University over his death.
The charges came after months of a grand jury investigation, which included video from surveillance cameras, testimony and phone records from Mr Piazza's final hours inside the fraternity house.
The report concluded that there was an attempt to conceal evidence of hazing - the initiation ceremony - and underage drinking after Mr Piazza was in hospital.

Syria war: US to arm Kurds in battle for Raqqa

A member of the US-backed Syrian Democratic Forces monitors the town of Tabqa, on April 30, 2017Image copyrightGETTY IMAGES
Image captionThe SDF is pressing IS back in the key city of Tabqa
US President Donald Trump has approved supplying weapons to Kurdish forces fighting so-called Islamic State (IS) in Syria, the Pentagon says.
Kurdish elements of the Syrian Democratic Forces (SDF) would be equipped to help drive IS from its stronghold, Raqqa, a spokeswoman said.
The US was "keenly aware" of Turkey's concerns about such a move, she added.
Turkey views the Kurdish rebels as terrorists and wants to stop them taking more territory in Syria.
The SDF, which comprises Kurdish and Arab militias, is already being supported by elite US forces and air strikes from a US-led coalition.
The group is currently battling IS for control of the city of Tabqa, an IS command centre just 50km (30 miles) from Raqqa.
A Pentagon source told the BBC the equipment would include ammunition, small arms, machine guns, heavy machine guns, construction equipment such as bulldozers and armoured vehicles.
The source added that the US would "seek to recover" the equipment afterwards.

Analysis: Gary O'Donoghue, BBC News, Washington

The US believes the Kurdish fighters - known as the YPG - will be essential to the city's downfall.
The Pentagon sees them as the most disciplined and organised of the anti-IS groups but Turkish opposition has meant Washington has had to tread a fine line.
The imminence of the fight for Raqqa means delay is no longer an option and the Kurds will be getting a range of equipment.
US sources say they have received assurances from the Kurds that they will leave Raqqa to be governed by Syrian Arabs after the battle.
Turkey's President Erdogan is due in Washington next week - he will not be a happy visitor.

No timeline has been given for when the weapons would start to be supplied.
"We are keenly aware of the security concerns of our coalition partner Turkey," said Pentagon spokeswoman Dana White, who is travelling with US Defence Secretary Jim Mattis in Lithuania.
"We want to reassure the people and government of Turkey that the US is committed to preventing additional security risks and protecting our Nato ally."
Turkey sees the Syrian Kurds as an extension of the PKK separatist group inside Turkey which has been designated a terrorist organisation by the US and EU.

Monday, May 8, 2017

LIVE: Kuagwa kwa miili ya watoto na walimu wa shule Lucy Vicent Arusha


Mourinho aigwaya Arsenal game ya leo!

Wakati Manchester na Arsenal wakitarajiwa kukutana jioni ya leo katika Uwanja wa Emirates kwenye mechi ya Premier League, Jose Mourinho amesisitiza kuwa mpinzani wake huyo atafurahi kutokana na yeye kupanga kuchezesha kikosi dhahifu leo
"Yeye (Wenger) ukweli atanifurahia kwa sababu nitabadilisha timu yangu dhidi ya Arsenal," alisema Mourinho. "Tunapaswa kuwa na ubinadamu na kwa wachezaji.
Tunapaswa kuwa na busara na (kuwatumia) kwa akili katika uhusiano kwa hali yetu ya Premier League. Mechi yetu ya mwisho dhidi ya Swansea ilikuwa ya mwisho kwetu kupigania nne-bora, hivyo nitapumzisha wachezaji wangu.
"Hatutakwenda Arsenal kusema “tufungwe tano ama 6-0”. Tunakwenda pale kupigania matokeo.
"Lakini siwezi sasa kuchezesha timu ile ile ambayo ilicheza Hispania na Celta Vigo halafu irudie tena Alhamisi ijayo."

Serikali yagharamia msiba wa Arusha


Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania imegharamia Sanda pamoja na majeneza kwa ajili ya Wanafunzi wa Shule ya Lucky Vicent waliopoteza maisha mapema jana kwenye ajali iliyokuwa ikihusisha safari ya kimasomo.
Akitoa taarifa hiyo leo Meya wa Jiji la Arusha , Mh. Calist Lazaro amesema kuwa taarifa za awali zinaonyesha kuwa tayari Serikali imekwishalipia gharama za majeneza na sanda ya kuhifadhia miili ya marehemu ambao kesho wanatarajiwa kufanyiwa ibada katika Uwanja wa mpira wa Sheikh Amri Abeid.
Aidha, Mh. Lazaro amesema kuwa viongozi mbali mbali wakiwemo mawaziri pamoja na wabunge bado wanaendelea kukusanyika katika eneo la shule ya Lucky Vicent  kwa ajili ya kikao na baadae majira ya saa tisa au kumi taarifa rasmi ya serikali itatolewa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha.

Yanga yarudi kileleni VPL

Tokeo la picha la yanga

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Young Africans wametoka vifua mbele baada ya kuwachapa mabao 2-0 wapinzani wao Tanzania Prisons katika mchezo uliochezwa uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.
Mabao hayo yote mawili yamepatikana katika dakika 45 za kipindi cha pili cha mchezo huo ambapo ilipofika dakika 71 Amisi Tambwe aliweza kuchungulia nyavu za wapinzani wao kwa mara ya kwanza na kuifanya Yanga kuongoza bao 1-0 na ilipofikia dakika 76 za mchezo Obrey Chirwa aliwainua tena mashabiki wa klabu hiyo kwa kufunga bao la pili na kuifanya timu yake kuibuka kidedea mpaka mpira kuisha.
Kwa matokeo hayo timu ya Yanga imeweza kujiongezea pointi zake 3 na kuifanya kufikia alama 59 sawa sawa na Simba SC.
Katika hatua nyingine Nahodha wa Prisons, Benjamini Asukile amesema pamoja na kufungwa na Yanga bado hawajakata tamaa na Prisons lazima itabaki Ligi Kuu Bara.
“Kuna makosa tulifanya kipindi cha pili na Yanga wakaitumia nafasi hiyo. Lakini tutaendelea kupambana na imani yetu Prisons itabaki ligi kuu”. Alisema Asukile

MUSIC