Tuesday, July 4, 2017

Rasmi John Terry ajiunga Aston Villa

HATIMAYE baada ya kuambiwa hatoongezewa mkataba na klabu aliyoichezea kwa muda mrefu nahodha wa zamani wa Chelsea na England John Terry amesaini kuichezea klabu ya Aston Villa inayoshiriki Championship licha ya kuwa na umri wa miaka 37.

Mmiliki na Mwenyekiti wa Villa Dr Tony Xia alithibitisha kuwasili kwa staa huyo aliyepata mafanikio makubwa akiwa na Chelsea Jumatatu asubuhi, akiandika kwenye Twitter yake: ‘Karibu JT Birmingham city…Aston Villa! #UTV! @AVFCOfficial!’

Kuwasili kwa Terry ambaye alikuwa anawindwa pia na mahasimu wa Villa, Birmingham City kuliwafanya mashabiki wa klabu hiyo kuanzisha group maalumu la WhatsApp kwa ajili ya kumkarubisha.


No comments:

MUSIC